Maneno mengine ya T B Joshua mwaka mmoja baada ya Jengo la Kanisa lake kuanguka..
Umepita mwaka mmoja sasahivi toka litokee tukio la kuanguka kwa Jengo la Kanisa la Synagogue Church of All Nations Nigeria ambalo linaongozwa na Mchungaji T B Joshua…
kuna watu wengi walifariki katika tukio hilo na ilikuwa stori ambayo
iligusa watu wengi kwa sababu ya umaarufu wa Mchungaji huyo nje ya
mipaka ya Nigeria.
T B Joshua ameandika ujumbe unaogusa kumbukumbu ya tukio hilo, kwenye alichokisema kuna haya maneno pia >>> ‘Ni
muhimu kukumbuka kwamba sisi ni Familia ya MUNGU, wakati mwingine
kwenye mazingira kama haya tunatakiwa kumuachia MUNGU… Tunatakiwa
kuamini kwamba vifo vya ndugu zetu ilikuwa ni mapenzi ya MUNGU, na
haikuwezekana kupingana nao‘- T B Joshua.
Ajali ya kuanguka kwa Jengo la Kanisa
hilo ilitokea September 12 2014, ambapo watu 115 walifariki na 84 kati
yao walikuwa Raia wa South Africa.
Watu na Rekodi zao… Huyu kavuta Ndege kwa kutumia masikio yake tu !!
Johnny Strange kutoka Uingereza, umri wake ni miaka 26, jina lake linaandikwa kwa wino mzito kwenye Kitabu cha Kumbukumbu kubwa Duniani, Guinness World Records baada ya kuandika Rekodi ambayo watu wengi wamebaki vinywa wazi wakimshangaa.
Strange kayafanya
maajabu yake na Dunia itamkumbuka kwa rekodi nyingi alizowahi
kuziandika ikiwemo hii mpya ya kuvuta ndege kwa kutumia masikio yake !!…
YES, haikuwa kazi rahisi kwake lakini tayari ameikamilisha na Rekodi
yake imeingizwa kwenye Kitabu cha Kumbukumbu za Guinness cha mwaka 2016.
‘Haikuwa
kazi rahisi kufanikiwa kuandika Rekodi hii… Ninafurahia sana kuandika
Rekodi mpya kila wakati na jina langu kuandikwa kwenye Kitabu cha
Guinness, yani mpaka nakosa sehemu ya kutundika vyeti vyangu sasahivi‘– Johnny Strange.
Ndege ambayo jamaa kaivuta ina uzito wa
Kilo 670, na amefanikiwa kuivuta Ndege hiyo kwa umbali wa kama Mita 20
hivi… hii inakuwa ni mara ya nane kwake kuvunja rekodi na jina lake
kuingia kwenye Kumbukumbu za Kitabu cha Guinness, rekodi ya kwanza
aliivunja akiwa na umri wa miaka 10 tu.
0 comments :
Post a Comment