Nuru The Light karudi na video yake mpyampya, inaitwa ‘L’… ni kazi ya Director Adam Juma…
Nuru The Light
ni moja ya mastaa ambao wana nafasi zao kutambulika kwenye muziki wa
Bongo Fleva, kuna kipindi kirefu hajasikika… haikumaanisha kauacha
muziki.
Nuru anarudi tena, muziki una mchakamchaka sasahivi, ataweza kushika?? kaachia video ya ngoma yake mpya ambayo kaipa jina la ‘L’ .
Milango imefunguka sana mastaa wa Bongo kufanya Video zao nje ya TZ sanasana South Africa… Nuru hajavuka huko, kaiamini kazi ya Director Adam Juma wa Visual Lab Tanzania, Video hii yote imekamilika kwenye mikono yake !
Baada ya kumaliza beef na Drake, Meek Mill anamtafuta Future…!?
Meek Mill kwenye headlines kwa mara nyingine tena, na kwa muonekano inaonekana kama Meek Mill bado hajatosheka na beefs na pengine time hii anataka kuanzisha beef lingine na msanii mwenzake wa HipHop Future!
Kwenye performance ya tamasha la ‘Made In America Festival’ siku ya jumapili September 6 jijini Philadelphia, Meek Mill alimzuia DJ wake kupiga nyimbo za Future na kumuamuru atoe nyimbo zote za Future kwenye playlist yake.
>>>“Oya
jamaa vipi wewe, unapiga sana ngoma za Future usiku huu… Kwani Future
ndio msanii pekee anayerap?! Wewe vipi bwana… emu acha hizo na piga
ngoma nyingine kali, huyo future bwana imetosha!!” <<< Meek Mill alisema baada ya kukerekwa na nyimbo hizo.
Hakuna anayejua kwanini Meek Mill aliamua
kumwambia DJ wake hivyo, na hakuna anayejua kwa nini nyimbo hizo
zimesababisha kikwazo kwa rapper huyo… imepita mwezi tu toka Meek Mill na Drake wamalize beef lao, pengine Meek anataka aanzishe lingine na Future!
Wewe unaonaje?
Diamond Platnumz ametaja tarehe atakayoonekana sura mtoto wake (Tiffah)
Hii ndio Shopping Mall iliyopewa jina la rais Jakaya Mrisho Kikwete 88.1 (Mwanza)
Stori ninayokusogezea sasa hivi ni hii
kutokea 88.1 Mwanza kuhusu Shopping Mall mpya inayotarajiwa kufunguliwa
wakati wowote ambayo itakuwa ikiitwa jina la rais wa jamuhuri ya
Muungano wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete.
Kwa mujibu wa afisa mahusiano wa jiji la Mwanza alipokutana na ripota wa millardayo.com..‘Tumeamua
kuita Jakaya Mrisho Kikwete kwasababu ni utamaduni wa muda mrefu kwa
kweli za utamaduni kwamba inapotokea kiongozi akafanya jambo jema na ni
zuri basi vitu uwa vinaitwa kwa jina lake ukaona kuna baadhi ya barabra
zimepewa majina kama ya Kenyatta,Nyerere’ – Joseph Mlinzi
‘Katika hili la Jakaya Mrisho Kikwete
Shopping Mall ni kwa utambuzi kwamba huyu ni rais wa jamhuri wa Muungano
wa Tanzania ambaye ameongoza kwa awamu mbili mfululizo ameweka mchango
mkubwa katika nchi yetu kipindi cha utawala wake ikiwa pamoja na
utekelezaji mzuri kupitia chama cha Mapinduzi’ – Joseph Mlinzi‘Shopping Mall hii ni kubwa kwa Afrika Mashabiki na kati kwa mfano ukienda Dar Mlimani city ambayo ina mita za mraba 15000, ukienda Kenya wana Westgate ambayo haifiki mita za mraba 30000, ukienda za Uganda na sehemu zingine, mwisho wa siku tulitaka kufanikisha yale maono ya Mheshimu Rais kwamba katika jiji la mwanza tunaona kitu kizuri bora na kinaelekea kule ambako yeye alisema anataka jiji la mwanza liwe kama California ya Tanzania’ – Joseph Mlinzi
Nimekusogezea list ya viongozi wanaolipwa pesa nyingi duniani…
Ninayo list ya viongozi wa mataifa
mbalimbali duniani wanaoongoza kwa kulipwa pesa nyingi , taarifa
ikufikie kwamba anayeshika nafasi ya tano ni Michael D. Higgins ambaye ni rais wa jamhuri ya Ireland, nafasi ya nne inashikwa na waziri mkuu wa Australia Tony Abbott, nafasi ya tatu inashikwa na rais wa Marekani Barack Obama, nafasi ya pili inashikwa na kiongozi wa Hong Kong Leung Chun-ying mshahara wake unauzidi mshahara wa rais wa China.
Nafasi ya kwanza wanasema katika
viongozi wa mataifa mbalimbali duniani anayelipwa pesa nyingi ni waziri
mkuu wa Singapore Lee Hsien Loong.
Waziri Mkuu huyo ndio kiongozi wa taifa
anayelipwa kwa mshahara mkubwa duniani akiwa analipwa dola za kimarekani
milioni 1 na laki 7.
Mashtaka dhidi ya Masha batili?, Karatasi za kura September 29, Sheria za kampeni… vivutio vya utalii CNN na BBC!?
Inawezekana ulikuwa kwenye foleni na uchambuzi wa magazeti @CloudsFM umekupita, kazi yangu siku zote ni kuhakikisha zile zote kubwa za asubuhi hazikupiti…
Mgombea Urais wa CHADEMA Edward Lowassa asema hakuta kuwa na muda wa kupoteza, ataanza kufanyia kazi ahadi zote alizotoa baada ya kuapishwa, Mgombea Urais wa CCM John Magufuli asema kama akichaguliwa kua Rais hakutakuwa na maadhimisho ya siku ya maji.
Mgombea Ubunge wa ACT Wazalendo jimbo la Chilonwa, Eva Mpagana amewaomba wananchi kumteuwa ili aweze kutatua tatizo la mawasiliano, Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Ernest Mangu amesema hakuna Sheria inayozuia wagombea Urais, Ubunge na Madiwani kufanya kampeni zaidi ya saa kumi na mbili jioni.
Chama cha TPP kimeonywa kuhusu kuendelea na kampeni, Lawrence Masha adai mashtaka dhidi yake ni batili, Rais mstaafu Benjamin William Mkapa anategemea kuzindua kampeni za CCM Bukoba.
Karatasi za kura kutua September 29 , vivutio vya Utalii nchini kurushwa kwenye vituo vya CNN na BBC wakati wowote kuanzia sasa, Waalifu wawili watoroka kwenye kituo cha polisi, Sheikh mkuu wa Dar es salaam Alhaj Musa Salum asema mchakato wa kumpata Mufti mkuu wa Tanzania kufanyika ndani ya siku 90.
Mfanyabiashara afikishwa Mahakamani baada ya kuingiza samaki nchini kutoka China bila kuwa na kibali maalum.
0 comments :
Post a Comment