Siku moja baada ya ushindi Lewis Hamilton kaonyesha gari lake la kifahari (Pichaz)
Bingwa wa mbio za magari ya Formula One Lewis Hamilton ameonekana akiwa na gari la kifahari kitu kinachotafsiriwa kama sehemu ya kusherehekea ubingwa wake wa hivi karibuni. Hamilton alishinda ubingwa wake wa saba wa msimu siku ya jumapili Monza Italia Grand Prix.
Siku moja baada ya ushindi wa Lewis Hamilton amepigwa picha akiwa na gari la kifahari la Mercedes G63 AMG ambalo thamani yake inatajwa kufikia pound 370,000 ambazo ni zaidi ya bilioni 1 ya Kitanzania. Tukio la Lewis Hamilton kupiga picha akiwa na gari hiyo inatafsiriwa kama ishara ya kusherehekea ubingwa wake.
Kuelekea michuano ya EURO 2016 Uingereza kufikia katika hotel hii ya kifahari (Pichaz)
Ni kawaida sehemu ambayo hutarajia
kupokea watu wengi katika kipindi fulani, bidhaa na vitu vingine
hupatikana kwa gharama za juu sana, kutokana na mkusanyiko wa watu wengi
na kama unahitaji baadhi ya huduma za sehemu hiyo kama hotel, vyakula
na vingine kwa urahisi lazima ufanye booking.
Timu ya taifa ya Uingereza imeshaanza kufanya maandalizi ya michuano ya EURO 2016 itakayofanyika Ufaransa, Uingereza imefanya booking ya hotel
na kuomba kupata huduma maalum kipindi watakapokuwa hapo, sambamba na
gharama ya pound 500 kwa usiku mmoja ambayo ni zaidi ya Tsh milioni 1.6
za Kitanzania kwa chumba.
Huduma watakazo pata Uingereza za VIP ni pamoja na huduma ya treni, uwanja wa mazoezi pamoja na ulinzi kwa usalama wa timu yao. Tayari shirikisho la soka Uingereza FA kupitia kwa kocha wa timu hiyo Roy Hodgson limethibitisha kufikia katika hotel ya Auberge du Jeu Paume na kuomba kupata huduma za VIP.
Uwanja
wa US Chantilly utakarabatiwa kabla ya timu ya taifa ya Uingereza
kufika hapo . Mwendo wa dakika 4 kutoka mahali watakapo fikia
Kocha wa timu ya taifa ya Uingereza Roy Hodgson kulia sambamba na msaidizi wake Gary Neville
Vincent Kompany kamchezea faulo binti yake Sienna
Vincent Kompany amezaliwa kuwa mshindi na kiongozi katika mchezo wa soka, Kompany ambaye ni nahodha wa klabu ya Manchester City pamoja na hayo, Kompany ni baba wa familia na anapenda kucheza na binti yake Sienna.
Nimeona nikukumbushe hii video ya nahodha huyo wa Man City akicheza na binti yake Sienna, licha ya kuwa hii video haikutoka mitandao, ilikuwa katika mechi ya msimu uliyomalizika baada ya mechi ya Man City dhidi ya Southampton mchezo uliyomalizika kwa Man City kuibuka na ushindi wa goli 2-0.
Kinachovutia wengi katika hii video ni jinsi nahodha huyo wa Man City
anavyocheza na mtoto wake, kwani amezoeleka mara nyingi kuwa serious,
ila hii michezo ya kumchezea faulo binti yake inaweza ikaja kumtoa meno.
Hii ni video ya tukio la nyuma ila imeonekana mitandao hivi karibuni.
Steven Gerrard akiwa na familia yake, moja kati ya sehemu zinazotajwa kuwa na furaha duniani (Pichaz)
Kiungo wa kimataifa wa Uingereza na klabu ya LA Galaxy ya Marekani Steven Gerrard ameingia katika headlines baada ya kwenda kuenjoy na familia yake Disneyland. Gerrard na mkewe pamoja na mabinti zake watatu walienda kutembelea Disneyland kama sehemu ya kufurahia mapumziko yao.
Familia ya Steven Gerrard ilienda kutembelea Disneyland ikiwa ni wiki moja imepita toka watembelee katika studio ya Universal akiwa sambamba na mkewe Alex, pamoja na mabinti zake Lily-Ella, Lexie na Lourdes. Disneyland inatajwa kuwa moja kati ya sehemu zenye furaha duniani kwa mujibu wa mirror.co.uk.
Hata hivyo Gerrard aliyejiunga na klabu ya LA Galaxy akitokea katika klabu ya Liverpool, bado anaendelea kuenjoy na kutembelea maeneo tofauti tofauti ya Marekani akiwa na familia yake.
0 comments :
Post a Comment