Mtoto wa mchezaji bora wa dunia kutokea Brazil amejiunga na klabu hii ya Ureno….
Mtoto wa mchezaji wa zamani wa FC Barcelona na timu ya taifa ya Brazil Rivaldinho Rivaldo ambaye anafuata nyayo za baba yake Rivaldo katika soka, amesajiliwa na klabu ya Boavista ya Ureno akitokea klabu ya Mogi Mirim ya kwao Brazil. Hivyo hiyo inakuwa mwanzo wa safari yake ya kusaka mafanikio kama aliyoyapata baba yake Ulaya.
Rivaldinho ambaye ana umri wa miaka 20 amejiunga na klabu ya Boavista
kwa mkataba wa miaka mitatu na kuhama katika klabu ambayo baba yake
mzazi ni Rais, hiyo itamfanya kukua na kukomaa kisoka kwani ataanza
kuishi mbali na uangalizi wa baba yake.
Mchezaji huyo ambaye amepata umaarufu
kutokana na ukubwa wa jina la baba yake, ni kawaida kuingia katika
headlines kila mara anapofunga goli, ameichezea klabu ya Mogi Mirim jumla ya mechi 44 na kufunga goli 10. Rivaldinho ili aweze kufikia rekodi za baba yake inabidi ajitume kwani hadi sasa hajawahi cheza katika timu ya taifa ya Brazil hata ya vijana.
Ujenzi wa Uwanja mpya wa Chelsea utafanana kitu hiki na Uwanja wa Taifa Dar Es Salaam (Pichaz)
Klabu ya Chelsea ya Uingereza
imeonyesha muonekano wa uwanja wao mpya ambao hadi mwaka 2020
inaripotiwa ujenzi wa uwanja huo utakuwa umekamilika. Bado mashauriano
yanaendelea kuhusiana na wakazi wa eneo husika utakapo jengwa uwanja
huo.
Mpango wa mmiliki wa klabu ya Chelsea Roman Abramovich ni kutumia pound milioni 500 katika ujenzi wa uwanja huo ili uwe biashara tofauti inayojitegemea mbali na Chelsea. Ujenzi huo ambao unatarajiwa kuanza baada ya miezi 9 kutokea sasa utaifanya klabu ya Chelsea kuhama uwanja wao wa Stamford Bridge na kutumia Uwanja wa Wembley kwa kipindi cha misimu mitatu.
Ujenzi huo wa Uwanja mpya wa Stamford Bridge utakuwa na uwezo wa kuchukua mashabiki 60,000 sawa na uwanja wa Taifa wa Dar Es Salaam, ambapo uwanja wa sasa wa Chelsea unachukua watu wasio zidi 41,000.
Huu ni muonekano wa sasa wa Uwanja wa Stamford Bridge
Pichaz za baadhi ya mastaa waliowasili katika timu zao za taifa, Ronaldo, Depay na Sanchez wapo pia..
Wiki hii ni wiki ya mechi za kimataifa kwa upande wa bara la Ulaya wao timu zao za taifa zitakuwa na mechi za kuwania kufuzu kucheza michuano ya Euro2016, ila kwa upande wa Afrika timu za taifa zitacheza michezo ya kuwania kufuzu katika michuano ya AFCON 2017.
Cristiano Ronaldo tayari yeye ameshajiunga na timu yake ya taifa ya Ureno na kuanza mazoezi. Timu ya taifa ya Ureno yenyewe itacheza mechi moja ya kirafiki siku ya Septemba 4 dhidi ya timu ya taifa ya Ufaransa kabla ya kusafiri kwenda kucheza mechi na Albania ya kuwania kufuzu Euro 2016.
Alex Sanchez naye amejiunga na timu yake ya taifa ya Chile kujiandaa na mechi za kimataifa za kirafiki ambazo zipo katika kalenda ya FIFA alipiga picha na kuweka katika mtandao wa twitter. Chile wataikaribisha Paraguay siku ya Jumamosi ya Septemba 5.
Sababu ya kushindwa kusajiliwa De Gea Real Madrid na maamuzi ya klabu hiyo kwa FIFA viko hapa…
Golikipa wa kimataifa wa Hispania ambaye anaichezea klabu ya Manchester United David De Gea, alikuwa akihusishwa kujiunga na klabu ya Real Madrid ya Hispania, hivyo kila kitu kilikuwa kimesha kuwa sawa ikiwemo maslahi binafsi ya mchezaji.
De Gea ambaye aliripotiwa usiku wa August 31 kuwa karibu na kujiunga na Real Madrid timu aliyokuwa akihusishwa kujiunga nayo tokea zamani, mpango wa De Gea kujiunga na timu hiyo ulikwama baada ya viongozi wa Man United kuchelewa kutuma mikataba katika klabu ya Real Madrid, hivyo walituma dakika moja baada ya dirisha la usajili kufungwa.
Tatizo la kuchelewa kwa documents za mikataba hiyo ni mfumo wa usajili wa FIFA ndio umefanya documents kutoka klabu ya Man United kuchelewa kufika kwa Real Madrid, kutokana na Real Madrid kuwa na ushaidi wa hizo documents watakata rufaa FIFA ili wapewe nafasi ya kumsajili De Gea nje ya muda wa usajili kwani mfumo wa FIFA ndio uliochelewesha usajili huo.
Klabu ya Real Madrid ya Hispania na Man United walikuwa wamekubaliana kuuziana golikipa huyo kwa ada ya pound milioni 29 pamoja na kupewa golikipa Keylor Navas, kama rufaa yao haitashinda watalazimika kusubiri hadi dirisha dogo mwezi January, dirisha la usajili kwa upande wa Hispania na Ufaransa tayari yashafungwa.
0 comments :
Post a Comment