Mabibi na mabwana ile single mpya ya Sauti Sol ndio hii imetoka
Ushauri wa Arsene Wenger kwa Thierry Henry kama anataka kupata mafanikio katika ukocha…
Kocha wa klabu ya Arsenal ya Uingereza Arsene Wenger ambaye amewahi kumfundisha Thierry Henry kama mchezaji wake kwa miaka mingi, Wenger amemshauri Thierry Henry kama kweli ana nia ya dhati ya kutaka kupata mafanikio kama kocha katika soka.
Wenger amemshauri Henry ambaye kwa sasa anaifundisha timu ya Arsenal
chini ya umri wa miaka 18 kuwa, kama kweli anataka kupata mafanikio
katika ukocha inabidi apate ushauri wa kisaikolojia katika akili yake. Henry anafundisha kikosi hicho cha vijana huku akipata mafunzo ya ukocha.
Henry ambaye anaheshima ya kuwa mfungaji bora wa klabu ya Arsenal kwa muda wote, alisajiliwa na Wenger akitokea klabu ya Juventus ya Italia mwaka 1999 ila Wenger amemueleza utofauti uliyopo kati ya kuwa mchezaji na kuwa kocha.
Picha 10 kutoka uwanja wa Tangamano Tanga kwenye kampeni za Urais za Mh.John Magufuli
Nimekusogezea na hizi nyumba 10 kali zilizojengwa ndani ya maji mtu wangu…(Pichaz)
Leo nimekusogezea hizi nyumba ambazo zimekuwa zikitumiwa na watu bila wasiwasi wowote huku zikiwa zimejengwa kitaalamu zaidi ndani ya maji.
Ninayo good news kutoka kwa bondia Francis Cheka iko hapa….
Unakumbuka ile ishu ya bondia wa ngumi Francis Cheka ya kumpiga na kumuumiza meneja wa baa yake akimtuhumu kusababisha hasara?
Sasa good news ninayotaka kukusogezea ni
kwamba bondia huyo wa mchezo wa masumbwi akiwa anatumikia kifungo cha
nje kwa sasa anatarajia kwenda nchini Uingereza tarehe 15 mwezi huu
kwenye mchezo wa masumbwi.
Leo sept 8 alikuta na ripota wa
millardayo.com na kuzungumza machache kuhusiana na taratibu za safari
yake pamoja na kifungo anachotumikia nje…’Kwanza
namshukuru mwenyezi mungu niko katika hali ya salama kesi yangu katika
ustawi wa jamii inaendelea vizuri na ustawi wa jamii niko nao katika
hali ya kawaida sababu wao wanajua umuhimu wangu na kuweza kujua mimi
Francis Cheka nahitaji nini kwa mashabiki wangu, mimi ni mtanzania
ambaye ninawajenga umma wa watanzania kwenye michezo ya boxer’ – Francis Cheka
‘Ustawi wa
jamii wamenipa ruksa ya kwenda kupigana kwenye pambano hilo nchini
Uingereza nategemea kwenda tarehe 15 mwezi huu na mkurugenzi wa ustawi
wa jamii ameweza kuniambia mawili matatu kuhusiana na taratibu au kitu
gani ninachotakiwa kukifanya ili niweze kufanikisha safari yangu ya
Uingereza’ – Francis Cheka
Kuhusu Kipre Bolou, hali ya Shomari Kapombe na Allan Wanga viko hapa kuelekea mechi ya Jumamosi
Wakati shirikisho la soka Tanzania TFF likithibitisha kuanza kwa Ligi Kuu soka Tanzania
bara siku ya Jumamosi ya September 12 na kudai mpango wa kuwataka
vilabu viwalipie wachezaji wa kigeni dola 2000 upo pale pale. Kwa upande
wa Azam FC kupitia kwa afisa habari wake Jafari Iddi Maganga amethibitisha kurejea kwa wachezaji wao.
Awali klabu ya Azam FC katika mchezo wa Ngao ya Hisani iliwakosa wachezaji wake wawili Kipre Bolou aliyekuwa majeruhi na Allan Wanga ambaye alifiwa na mama yake mzazi. Wanga amerejea baada ya kukosekana kwa kufiwa na mama yake na kuitumikia timu yake ya taifa ya Kenya.
“Kipre
Bolou ambaye alikuwa ameenda Cape Town kwa matibabu, amerejea jana usiku
tumempokea na alienda kule kwa ajili ya matibabu yake na tutakuwa naye
kwa muda wa mwezi mmoja akiangalia afya yake na wakati huo huo
akiandaliwa kucheza katika Ligi Kuu” >>> Jafari Iddi Maganga
“Utaratibu
wa madaktari ni kwamba amekwenda wameangalia afya yake na wamesema kuwa
hawawezi kumfanyia upasuaji kutokana na hali aliyokuwa nayo lakini
wametoa maelekezo kwa madaktari wetu kitu gani kwamba anapaswa kufanyiwa
ili aweze kurudi uwanjani”>>> Jafari Iddi Maganga
Comedy
Kipaji kingine cha mbwa… jamaa akaona amtumie kumshikia wine yake…
Lakini kwa wenzetu mbwa amekuwa sehemu ya familia na wamekuwa wakipewa huduma zote ambazo binadamu wengine wanazipata.
Wako wengine ambao hutumia gharama kubwa kuwatunza mbwa wao pamoja na kuwafundisha mambo mbalimbali.
Eve anaiyeishi Carlifonia,Marekani yeye aliamua kumfundisha mbwa wake jinsi ya kubalance glass yenye wine kichwani huku akiwa hana wasiwasi wowote.
Tazama hapa alichofanya…
Nimekuwekea na video yake kabisa mtuwangu…
0 comments :
Post a Comment