Wapo watu hata nchini Tanzania wamefanya ubunifu mzuri sana, matumizi ya kwanza kabisa ya Makontena ni kusafirishia mizigo kwenye meli, ndege au hata kwenye malori makubwa ya mizigo.
Lakini kuna maeneo ukikatisha mitaani unakuta wako watu ambao wameamua kuyatumia makontena kwa ajili ya biashara, yani kuna maduka, mini supermarkets za nguvu kabisa zimefunguliwa kwenye Kontena ambalo tayari limefanyiwa ufundi na linapendeza kama ujenzi wa maduka mengine unavyokuwa.
CRG Architects ni Kampuni yenye makazi yake China, waliingia Mumbai India kwa kazi moja tu.. kukamilisha ujenzi wa ghorofa za Containskyscraper ambazo kwenye ujenzi wake wote kilichotumika ni makontena tu !!
Ujenzi wote umekamillika kwa kutumia jumla ya makontena 2,400 na hapo itakuwa makazi ya watu zaidi ya 5,000 ambao hawana uwezo na wanaishi kwenye nyumba zilizosongamana na mazingira yake sio salama.
Huu ni mchoro unaoonesha ubunifu ulivyokuwa mpaka ghorofa linakamilika.
0 comments :
Post a Comment