Maneno ya Diamond Platnumz baada ya kutajwa kuwania tuzo ya MTV Europe Music Awards 2015
Naseeb Abdul aka Diamond Platnumz
amepata nafasi ya kuipeperusha bendera ya Tanzania katika tuzo za MTV
Europe Music Awards 2015 zitakazotolewa mwezi October 25, 2015 jijini
Milani Italy.
Msanii huyo ambaye ametajwa kuwania tuzo
ya MTV Europe Music Awards katika kipengele cha Best African Act,
akiongea na ripota wa millardayo.com alisema..‘Kiukweli
namshukuru sana mwenyezi Mungu kwasababu najua mimi naamini sio mimi tu
watanzania wengi ndoto zenu ni kuomba muziki wetu uweze kutambulika
kimataifa sio tu kutambulika bali kupewa heshima kwa taifa letu la
Tanzania‘ – Diamond Platnumz
‘Kwasasa
mambo yanaenda vizuri kabisa kwa hiyo kuteuliwa katika tuzo za MTV
Europe kwangu ndio mara yangu ya kwanza pia hata kwa Tanzania,
namshukuru Mwenyezi Mungu nauzuri tuzo hizo haziangalii chochote kwani
zinaangalia kura za watu so naamini muda ukifika basi mashabiki tupige
sana kura ili tuweze kufanikiwe kuuleta ushindi nyumbani, nakumbuka
mwaka jana walishinda Sauti Sol‘ – Diamond Platnumz
Mo Music aliingia kwenye Muziki rasmi akiwa darasa la ngapi?, Baba yake kayajibu hapa
Najua nina watu wangu mnaotamani
kufahamu historia ya wasanii pindi bado hawajajulikana katika tasnia ya
sanaa ukiwa na amu ya kufahamu tabia au kitu alichokuwa analichokuwa
anapenda msanii enzi za utoto wake.
Sasa basi ripota wa millardayo.com
amekutana na Baba mzazi wa Mo Music Martin Katemi na kuzungumza naye
kuhusu historia ya msanii Moshi aka Mo Music.
‘Mimi ni
Martin Katemi baba mzazi wa Moshi nyie mnamfahamu kama Mo Music nina
watoto wawili wa kiume yeye ni wa pili,kijana wangu enzi za utoto
alikuwa anapenda sana kukaa na makundi ya vijana wenzake na kuna muda
alikuwa anakuja nao marafiki zake nyumbani’ – Martin Katemi
‘Makundi yake walikuwa ni watu wa
kutengeneza vitu kama magari pia hata ufugaji wa Mbwa ni mpenzi sana wa
Mbwa kuna wakati alikuwa anajibishana sana na marafiki zake kuhusu
ufugaji wa Mbwa na alipofikia darasa la saba alikuwa na kundi la muziki
ambapo walikuwa wakienda mlimani hapa ulipo ukiangalia juu kuna eneo la
mlima unaitwa Mlima wa Papa’ – Matin Katemi‘Kule walikuwa wanafanya uimbaji lakini sisi wazee tulifanya kazi kubwa sana ya kuchuguza ni kitu gani wanachokifanya kwani kule ni eneo ambalo huwa wanakaa wahuni wavuta bangi na watu wengine lakini tulivyokwenda tukawakutana wana ma guitar na vifaa vya muziki baadae ndipo tukaanza kuona matunda kutoka kwa Mo Music baada ya kutoka wimbo wake wa kwanza’ – Martin Katemi
‘Na nyumbani kwao Mo Music ndio kando kando ya huo Mlima na ndio maana alikuwa akienda huko kwenda kufanya mazoezi yake na marafiki zake’ – Martin Katemi
Maneno ya Kalapina kuhusu pingamizi alilolipata dhidi ya mgombea mwenza…
Msanii huyo alikutana na ripota wa millardayo.com leo Sept 9, 2015 na kuzungumza kuhusu pingamzi alilolipata jimboni kwake dhidi ya mgombea mwenza kupitia chama cha Mapinduzi
‘Kiukweli niliwekewa pingamizi na
mgombea wa CCM Issa Mohamed akidai kwamba sija dhaminiwa na chama change
lakini nikawa nimetoa utetezi wa kutosheleza tu kwa msimamizi msaidizi
wa uchaguzi Salim Hassan Msuya wilayani Kinondoni na msaidizi wake
anaitwa Victor Muhenge’
‘Lakini kinachoonekana kwa mimi binafsi
na hata mtazamo wa chama changu ningependa kusema hiki watanzania wote
wajue kwamba pale kuna hujuma manispaa ya Kinondoni kwamba Iddi Hassan
anaonekana anashirikiana na watendaji wa pale katika ku engineer hizi
pingamizi za namna moja au nyingine’ – Kalapina
‘Kwasababu aliwekea pingamizi wagombea
wengi lakini kikuweli hazikuwa pingamizi zenye mashiko na naishukuru
ningependa kuishukuru tume ya uchaguzi na mkurugenzi wa tume kwa kuweza
kutupilia mbali pingamizi la mgombea wa CCM’- Kalapina
0 comments :
Post a Comment