Pichaz TBT za mastaa wako Kanye West, Jay Z,Chris Brown,Beyonce ninazo hapa mtu wangu…
Unaweza kuzitazama hapa mtu wangu..
John Legend
Nicki Minaj aweka historia Las Vegas, atajwa kuwa msanii wa kwanza wa kike wa hiphop kupewa zawadi hii…! (Pichaz)
Nicki Minaj ni mmoja kati ya wasanii wa kike kwenye muziki wa Hip Hop wanaofanya vizuri sana na wenye ushawishi mkubwa sana duniani.
Licha ya wimbo wake wa Anaconda kupokea tuzo ya Best Hip Hop Video VMA Award mwaka huu, Nicki Minaj amesherekea mwaka mmoja wa mafanikio ya wimbo huo kwa kupokea sanamu wake wa kwanza kabisa kwenye nyumba ya makumbusho ya Madame Tussauds Wax Museum iliyopo jijini Las Vegas.
Sanamu ya Nicki Minaj jijini Las Vegas Marekani kwenye nyumba ya makumbusho iitwayo Madame Tussauds Wax Museum.
Wazo la ‘sanamu’ huyo limetoka kwenye video ya wimbo wa ‘Anaconda’ na zawadi hii haijawahi kutolewa kwa msanii yoyote wa kike anayefanya muziki wa hipohop hivyo Nicki Minaj ni msanii wa kwanza wa kike kwenye muziki wa hiphop kuzawadiwa sanamu wake na nyumba hiyo ya makumbusho.
Nicki Minaj amefurahishwa sana na tukio hili huku akisema limemjia kama suprise kwake kwani hakutegemea kabisa kama kuna siku ingetokea Madame Tussauds Wax Museum kutengeneza samanu kwa ajili yake!
Hizi ni baadhi ya picha kutoka kwenye Instagram ya Nicki Minaj…
Hii ndio picha ambayo nyumba ya makumbusho ya Madame Tussauds Wax Museum ilitumia kutengeneza sanamu wa Nicki Minaj.
Picha
hii inamuonyesha sanamu wa Nicki Minaj kwa ukaribu… duh usipokuwa
makini unaweza kuhisi huyu ni Nicki Minaj kwenye pozi na sio sanamu!!
Mashabiki nao hawakuwa nyuma sana mtu wangu, yani fasta wakafika Las Vegas ili kupiga picha na sanamu la Nicki Minaj… na huyu kaka ameona bora amalize kila kitu hapa kwasababu pengine hatoweza kupata chance ya kuwa karibu kwa kiasi hiki na Nicki Minaj au hata chance ya kumshika…
Shabiki kwenye ubora wake mtu wangu!
Majibu ya Roma Mkatoliki baada ya single yake mpya kuzuiliwa kuchezwa kwenye vituo mbalimbali
Msanii huyo alipokutana na ripota wa millardayo.com aliweza kuelezea sababu zilizopelekea kuzuiliwa kwa single yake mpya iitwayo Viva Roma na kusema..’Kiukweli jana ndio ilikuwa tarehe 9 mwezi wa tisa ambayo nilitoa ahadi kwa watu kuwa nitaachia wimbo wangu mpya unaoitwa Viva Roma na asubuhi mapema kabisa kwenye ukurasa wangu wa instagram nilipost picha ikionesha napaki CD zangu nikiwa tayari kuisambaza kazi yangu mpya mimi na timu yangu nzima ya Tongwe Records; – Roma Mkatoliki
‘Ilikuwa saa saba nianze na Eatv Radio kwenye kipindi cha Planet Bongo, saa nane nitaenda XXL ya Clouds FM, halafu nitaenda Times FM, halafu nitaenda E FM, na Magic FM so nilikuwa natoa ratiba ya kuitambulisha wimbo wangu katika vituo mbalimbali vya radio’ – Roma Mkatoliki
‘Ila mpaka sasa tunavyoongea tumeshaisambaza katika vituo vyote mbalimbali sehemu ambayo bado ni kwenye mitandao tu kama blogs, website na nchi za jirani ila jibu nililopewa na baadhi ya vituo vya radio ni kwamba wameikataa kuicheza ngoma yangu kwasababu wanachodai kwamba ina maneno makali huku vituo vingine vikiwa vinacheza verse moja tu kiukweli imenisikitisha lakini kwa upande wa mashabiki wanasema wimbo ni mzuri na sio kama ninalaumu vituo vya radio ila ndio maamuzi yao – Roma Mkatoliki
Ishu ya Kassim Mganga kutapeli show Iringa ni kweli? Stori ipo kwa Soudy Brown..#Uheard
Soudy Brown leo kapiga Stori na DJ mmoja ambae amesema kwamba staa wa Bongo Fleva, Kassim Mganga ilikuwa akafanye show Iringa lakini tayari alikuwa amepewa hela kwa ajili ya show nyingine Njombe.
Wakati wakiwa hotelini walishangaa jioni Polisi wanakuja na kumkamata Kassim baada ya kuambiwa Kassim Mganga alikuwa tayari amelipwa laki 5 na alitaka arudishiwe gharama zake ambazo zilifika zaidi ya milioni 1 lakini hakuwa nazo.
DJ huyo amesema aliamua kumdhamini Kassim ili wasimfunge, lakini baada ya hapo jamaa hakuwa anapokea simu wala hajalipa hizo pesa mpaka sasa.
0 comments :
Post a Comment