Tayari Barcelona imemuongeza jamaa wa nne kwenye list ya manahodha wao..
Kiungo raia wa Argentina Javier Mascherano ameteuliwa
kuwa nahodha wa nne kwenye klabu ya Barcelona akiongeza idadi ya
manahodha ambayo ilikuwa imebakia manahodha watatu baada ya kuondoka kwa
Xavi Hernandez.
Kuondoka kwa Xavi Hernandez kumefungua nafasi moja ya unahodha baada ya kupandishwa kwa Andres Iniesta ambaye amekuwa nahodha wa kikosi cha kwanza huku Lionel Messi akiwa nahodha wa pili na Sergio Busquets akiwa nahodha wa tatu.
Kocha wa Barcelona, Luis Enrique amemzungumzia Mascherano
kama mchezaji ambaye ana sifa ya uongozi hata kama sio nahodha rasmi
kwenye timu na kwa sababu hii ana kila sifa ya kuwemo kwenye orodha ya
manahodha wa klabu.
Enrique ameongeza kuwa Mascherano ni mchezaji ambaye timu nzima inamheshimu na hivyo ni uchaguzi ambao haukuwa na pingamizi toka kwa wachezaji wengine.
Mapokezi ya Magufuli kuchukua Fomu na alivyosindikizwa mpaka ofisi za CCM
Agosti 4, 2015 ni siku ambayo mgombea wa
nafasi ya Urais kupitia CCM Dkt. John Pombe Magufuli tayari kafika
kwenye ofisi za Tume ya Uchaguzi Tanzania kuchukua fomu za kuwania
nafasi hiyo ya Urais 2015.
Hizi ni pichaz pamoja na maneno
waliyoongea Rais wa Jamhuri wa Muungaano Tanzania Dkt Jakaya Mrisho
Kikwete pamoja na mgombe wa urais kupitia CCM Dkt.John Pombe Magufuli.
0 comments :
Post a Comment