David Beckham anatarajiwa kucheza movie ya James Bond 007…
Staa wa zamani wa klabu za Real Madrid, Man United, LA Galaxy na timu ya taifa ya Uingereza David Beckham anatarajiwa kuonekana katika movie. Beckham mwenye umri wa miaka 40, imeripotiwa kwa mujibu wa mtandao wa mirror.co.uk, unamtaja David Beckham kucheza katika movie ya James Bond.
Beckham anatajwa kuchukua nafasi ya Daniel Craig ambaye mkataba wake unakaribia kumalizika, Beckham ambaye
ni baba wa watoto wa nne amekiri kuwa aliwahi kufikiria kucheza movie
baada ya mashabiki kushauri hilo . Hata hivyo taarifa hizi sio ngeni kwa
mashabiki wa Beckham kwani ameshawahi kukiri kushawishika katika masuala ya movie.
Daniel Craig
Pichaz za Neymar alipokutana na pacha wa mcheza tennis New York…
Winga wa kimataifa wa Brazil na klabu ya FC Barcelona ya Hispania Neymar ameingia katika headlines akiwa New York, Neymar ambaye yupo New York na timu yake ya taifa ya Brazil, ameingia katika headlines baada ya kupigwa busu na ndugu wa mcheza tennis kutokea Canada.
Beatrice ambaye ni pacha wa Eugenie Bouchard alipiga picha akimpiga busu staa wa Brazil Neymar wakiwa katika uwanja wa Red Bull Arena wakati ambapo Brazil walikuwa katika harakati za kucheza mechi ya kirafiki. Picha ambayo imekuwa stori katika mitandao ya kijamii.
Mcheza tennis wa Canada Eugenie Bouchard
Hadi July 2014 hawa ndio mastaa 12 wa soka wanaotajwa kuwa wakali wa mitindo (Pichaz)
Hadi July 2014 mtandao wa artbecomesyou.com ulikuwa unawataja mastaa kadhaa wa soka kuwa ndio wakali wa style
za mavazi. Licha ya watu wengi kuwa wanaamini kuwa ukiwa na fedha,
utakuwa unavaa sana pamba na mkali wa mitindo, ndio ni kweli ili
upendeze lazima uingie gharama, unaweza vaa vitu vya gharama lakini
usipendeze kutokana na mpangilio wako, ila mastaa hawa ndio wanaotajwa
kuwa wakali katika masuala ya mavazi.
- David Beckham jamaa ana nyota ya kupendwa kutokana na muonekano wake na ustaa wake kapewa nafasi ya kwanza katika masuala ya kupangilia pamba na mitindo.
2. Samuel Eto’o uhodari wake haukuishia uwanjani tu hata katika masuala ya mitindo huwa ni mkali pia.
3. Daniel Sturridge huyu ni mkali wakuzifumania nyavu katika soka, kwa suala la mitindo tu yupo vizuri.
4. Raul Meireles staa kutokea Ureno
anatajwa kama mgonjwa wa masuala ya mitindo na mavazi japo mavazi yake
mingine du!! watu hushangaa ila naye yumo katika hii list.
5. Cristiano Ronaldo tumezoea kumuona akiwa katika headlines kutokana na jina lake, kwa mavazi tu yupo vizuri.
6. Didier Drogba style yake ya nywele pekee inatosha kumjua kuwa ni mtu wa masuala ya kwenda na wakati (Fashion)
7. Thierry Henry heshima yake haijaishia katika klabu ya Arsenal na timu ya taifa ya Ufaransa, hata katika ulimwengu wa Fashion wanamtambua.
8. Mario Gomez anatajwa kuwa na muonekano wa models wa fashion hivyo jina lake na muonekano wake humfanya apate mikataba ya kutangaza nguo wakati mwingine.
9. Sergio Ramos yupo sawa na mchezaji mwenzie wa Real Madrid Cristiano Ronaldo, wote ni wakali katika masuala ya fashion.
10. Djibril Cisse ni staa kutokea Ufaransa, kwanza ana muonekano wa kipekee tofauti na wengine kuanzia style ya nywele, ndevu hadi mavazi.
11. Andrea Pirlo anatajwa kuwa akivaa mavazi mengine tofauti na mavazi ya soka unaweza usimtambue kwa muonekano wake aliyo nao.
12. Keisuke Honda mjapan pekee aliye bahatika kuwa katika hii list ya wakali wa style kwa muonekano na mavazi .
Hii ni list ya mastaa wa movie na soka wanaofanana, Di Maria, Messi na Kolou Toure wapo pia…
Kuna usemi unaosema duniani watu wawili
wawili kwa maana ya kuwa kila mtu duniani ana mtu aliyefanana naye.
Huenda ukawa hujawahi kuonana na mtu unayefanana naye ila huwa inaamika
kuwa yupo tu sema bado haijatokea bahati ya nyinyi kukutana. Septemba 6
nakusogezea hii list ya mastaa wa soka na filamu wanao fanana.
Fernando Torres kutokea Atletico Madrid anafananishwa na Sacha Baron Cohen
Hizi ni sababu za Memphis Depay wa Man United kuto tumia jina la baba yake katika jezi…
Winga mpya wa klabu ya Manchester United Memphis Depay
ameingia kwenye headlines, kama ambavyo huwa ni kawaida kwa mastaa
kuingia katika headlines za vyombo vya habari kutokana na maisha yao na
uwezo wao uwanjani, safari hii winga huyo wa Kiholanzi ameingia kwenye
headlines baada ya kugoma kutumia jina la baba yake.
Memphis Depay
mwenye umri wa miaka 21 amegoma kutumia jina la baba yake katika jezi
yake anayovaa, siku zote imezoeleka kuona wachezaji wengi hupenda
kutumia majina ya baba zao katika jezi au hata maofisini, ila hii ni
tofauti kidogo kwa winga huyo, kwani amegoma kutumia jina la baba yake,
kwa sababu alimuacha toka akiwa na umri wa miaka minne.
Baba yake kaomba msamaha kwa kosa hilo, Memphis bado hajajibu chochote ila baba yake alihojiwa na the sun na kumuomba mwanaye huyo wasahau mgawanyiko uliyokuwepo kati yake kwa miaka 17 iliyopita.
Didier Drogba hadhihirisha ubora wake Ligi Kuu Marekani
Mshambuliaji wa zamani wa klabu ya Chelsea na timu ya taifa ya Ivory Coast Didier Drogba, ambaye kwa sasa anaichezea klabu ya Montreal Impact inyoshiriki Ligi Kuu Marekani (MLS), ameanza vizuri katika mechi yake ya kwanza toka ajiunge na Ligi hiyo.
Drogba aliyejiunga na timu hiyo kama mchezaji huru baada ya kumaliza mkataba wake na Chelsea, alifanikiwa kuifungia timu hiyo goli 3 (hat-trick) katika ushindi wa goli 4-3 dhidi ya klabu ya Chicago Fire. Huo ni mwanzo mzuri kwa staa huyo wa Afrika katika Ligi Kuu Marekani.
Utundu wa Cristiano Ronaldo na Ricardo Quaresma katika ndege kabla ya kuelekea Albania (Pichaz)
Kikosi cha timu ya taifa ya Ureno kilisafiri Jumamosi ya September 5 kuelekea Albania kucheza mechi ya kuwania tiketi ya kucheza michuano ya Euro 2016. Mchezo utapigwa Jumatatu ya September 7, muda mchache kabla ya kuanza safari ya kuelekea Albania ambapo watafikia katika mji mkuu wa nchi hiyo Tirana.
Mshambuliaji wa klabu ya Real Madrid Cristiano Ronaldo pamoja na winga wa klabu ya Besiktas, Ricardo Quaresma waliingia
katika chumba cha rubani na kupiga picha na video, ambayo muda mchache
baadae ilianza kuenea katika mitandao ya kijamii, hii ilikuwa kabla ya
ndege kuanza safari ya kuelekea Albania.
Wayne Rooney kaweka rekodi hii mbele ya mkewe Coolen na mtoto wake Kai (Pichaz)
Kama ambavyo ilivyokuwa kwa upande wa bara la Afrika kuliwa na michezo kadhaa kupigwa weekend hii na bara la Ulaya ilipigwa michezo kadhaa ya kuwania kufuzu kucheza michuano ya Euro 2016. Timu ya taifa ya Uingereza Jumamosi ya Septemba 5 ilicheza mechi dhidi ya San Marino.
Nahodha wa Manchester United Wayne Rooney aliingia katika headlines baada ya kuifikia rekodi ya mfungaji bora wa muda wote katika timu ya taifa ya Uingereza Sir Bobby Charlton, rekodi ambayo inatajwa kudumu kwa muda wa miaka 45. Rooney aliifikia rekodi hiyo baada ya kufunga goli moja katika ushindi wa goli 6-0 dhidi ya San Marino.
0 comments :
Post a Comment