Matokeo ya Man Utd vs Liverpool nimekuwekea hapa

Ule mtanange uliokuwa unasubiriwa kwa hamu baina ya wapinzania wa jadi wa ligi kuu ya Uingereza, vilabu vya Manchester United dhidi ya Liverpool umepigwa usiku huu.

 
Mchezo huo uliopigwa katika dimba la Old Trafford umemalizika kwa Mashetani wekundu kuendeleza ubabe dhidi ya Liverpool kwa mara ya tatu mfululizo.
 
Daley Blind alianza kuifungia United goli la kwanza muda mfupi baada ya kipindi cha pili kuanza, kabla ya Ander Herrera kufunga la pili kupitia mkwaju wa penati.
Christian Benteke aliifungia Liverpool goli la kufutia machozi kwa mtindo wa ‘tik tak’ mwishoni mwa kipindi cha pili kabla ya mshambuliaji mpya wa Man United – Anthony Martial kufunga goli la 3 kwa United.
 

Hiki ndicho kilichowakuta Espanyol walipocheza na Real Madrid leo

Ligi kuu ya Uhispania imeendelea leo baada ya mapumziko ya kupisha mechi za kimataifa kumalizika, Real Madrid walisafiri mpaka jijini Barcelona kwenda kucheza na Espanyol.
 
Mchezo uliopigwa katika dimba la Cornella El Plat umeshuhudia mwanasoka anayeshikilia taji la uchezaji bora wa dunia Cristiano Ronaldo akifunga magoli 5 katika mchezo uliomalizika kwa Real Madrid kushinda 6-0.
 
Ilimchukua Cristiano Ronaldo dakika 20 tu kufunga hat trick katika dakika ya 7, 17 na 20, kabla ya Karim Benzema hajafinga goli la 4 katika dakika ya 28 na hivyo kupelekea Madrid kwenda mapumziko wakiwa mbele kwa 4-0.
 
Kipindi cha Ronaldo akaongeza magoli mawili katika dakika ya 60 na 80 ya mchezo huo na hivyo kukamilisha ushindi wa 6-0
Timu zilipangwa hivi
Espanyol: Lopez, Arbilla, Alvaro, Ciani (Paco Montanes 46), Duarte, Victor (Joan Jordan 64), Javi Lopez (Canas 46), Alvarez, Salva, Gerard, Caicedo
Substitutes not used: Bardi, Juan Fuentes, Raillo, Sylla
Booked: Alvaro, Canas
Real Madrid: Navas, Carvajal, Pepe, Ramos (Varane 74), Marcelo, Casemiro, Modric (Kovacic 55), Isco, Bale, Ronaldo, Benzema (Vazquez 62)
Substitutes not used: Casilla, Kroos, Arbeloa, Jese
Scorers: Ronaldo 7, 17 pen, 20, 61, 80; Benzema 28

Nimekusogezea matokeo ya Arsenal vs Stoke na Man City vs Crystal Palace 

Baada ya mchezo wa mchana kati ya Chelsea vs Everton, Barclays Premier League imeendelea kutimua vumbi kwenye viwanja tofauti nchini Uingereza.
 
Arsenal wakiwa nyumbani waliikaribisha timu ngumu ya Stoke City- mechi ambayo imemalizika kwa vijana wa Arsene Wenger kupata ushindi wa 2-0.
Magoli ya Arsenal yalifungwa na Theo Walcott na Oliver Giroud.
 
Manchester City wakicheza ugenini leo wamefanikiwa kuendeleza rekodi yao ya kushinda mechi zao zote za EPL kwa goli 1-0 dhidi ya Crystal Palace.


Tayari ninayo matokeo ya mechi ya African Sports Vs Simba (+Pichaz)

September 12 ndio siku ambayo pazia la Ligi Kuu Tanzania bara limefunguliwa kwa michezo kadhaa kupigwa katika viwanja tofauti tofauti, mchezo uliyokuwa umeteka hisia za watu wengi ni mechi kati ya African Sports dhidi ya Simba mechi iliyochezwa katika uwanja wa Mkwakwani Tanga.
Mvuto wa hii mechi unatokana na rekodi ya klabu ya Simba kwa hivi karibuni kutofanya vizuri katika mechi zake za Ligi Kuu alizocheza Tanga katika uwanja wa Mkwakwani. Huku kwa upande wa African Sports ndio wamerudi Ligi Kuu baada ya kushuka miaka kadhaa nyuma hivyo hawakuwa tayari kupoteza mechi yake ya kwanza ya msimu, tena katika uwanja wake wa nyumbani.
DSC_0161
Wachezaji wa African Sports wakimsukuma Mgosi baada ya kumfanyia faulo mchezaji mwenzao
Mechi imemalizika kwa klabu ya Simba kuondoka na ushindi wa goli 1-0 goli pekee lilifungwa na mshambuliaji wa kimataifa wa Uganda aliyewahi kuichezea Yanga Hamisi Kiiza, kipindi cha pili. Licha ya kukosa nafasi kadhaa Simba ilifanikiwa kutumia nafasi moja kutoka kwa nahodha wao Musa Mgosi na Kiiza kutia nyavu kwa kichwa.
DSC_0065
Ayoub Masoud akijaribu kumpita Peter Mwalyanza wa Simba
DSC_0067
Ayoub Masoud akiwania mpira na Peter Mwalyanza
DSC_0198
Benchi la klabu ya African Sports
DSC_0176
Hassan Kessy wa Simba akichuana na Rahm Abdallah
DSC_0197
Kocha wa African Sports Joseph Lazaro
DSC_0189
Simon Serunkuma akiingia kuchukua nafasi ya Mwinyi Kazimoto
DSC_0186
Kocha wa Simba Dylan Kerr akitoa maelekezo
DSC_0182
Rahm Abdallah akimtoka mchezaji wa Simba
DSC_0158
Nahodha wa Simba Musa Mgosi akipiga krosi
DSC_0173
DSC_0138
Musa Mgosi akipata huduma ya kwanza baada ya kupata maumivu
DSC_0135
Hamisi Kiiza akisali baada ya kufunga goli
DSC_0140
Mgosi akitoka nje baada ya kupata maumivi
DSC_0143
Musa Hassan Mgosi
DSC_0134
Wachezaji wa Simba wakishangilia goli huku mshika kibendera akiwarudisha uwanjani
DSC_0132
DSC_0087
Mzozo wa wachezaji baada ya kufanyiwa faulo mchezaji wa African Sports
DSC_0086
DSC_0074
DSC_0055
Golikipa wa African Sports Yusuph Yusuph akiokoa goli


Matokeo ya Chelsea vs Everton nimekuwekea hapa

Baada ya mapumziko ya takribani siku 14, ligi kuu ya England maarufu kama Barclays Premier League imeendelea mchana wa leo kwa mchezo mkali kati ya Chelsea dhidi ya Everton.
 
Mchezo huo uliopigwa katika jiji la Liverpool ndani ya uwanja Goodison Park umemalizika kwa Chelsea kuambulia kipigo kingine kwa kufungwa 3-1.
 
Magoli matatu ya mshambuliaji Naismith yametosha kuipa Everton ushindi mzito dhidi ya vijana wa Jose Mourinho.
 
Naismith alianza kufunga katika dakika ya 17, dakika 5 baadae akaongeza la pili kabla ya Matic hajaifungia Chelsea goli la kufutia machozi.
Dakika 8 kabla ya mchezo kumalizika Naismith akashindilia msumari wa mwisho na kuipa ushindi wa 3-1 Everton.

First Eleven ya African Sports Vs Simba (+Pichaz)

Dakika kadhaa kabla ya mchezo kuanza nakusogezea first eleven ya timu zote mbili.
African Sports mwenyeji wa mchezo huu
DSC_0046
Kikosi cha African Sports
  1. Yusuph Yusuph 30
  2. Ayoub Masoud 2
  3. Mwaita Gereza 21
  4. Juma Shemvuni 24
  5. Rahm Abdalah 26
  6. Novat Lufungo 22
  7. James Mendi 5
  8. Hussein Amir 4
  9. Hassan Matemema 10
  10. Omary Issa 16
  11. Pera Mavuo 7
Wachezaji wa akiba
  1. Zacharia Mwaluko 1
  2. Alfani Twenye 23
  3. Ally Ramadhani 13
  4. Mussa Chambe 6
  5. Bakari Masoud 20
  6. Victor Hangaya 23
  7. Nzara Ndaro 19
Kikosi cha Simba kitakachoanza leo ni
DSC_0044
  1. Peter Manyika
  2. Mohamed Hussen
  3. Hassan Kessy
  4. Juuko Murishid
  5. Justice Majbavi
  6. Awadh Juma
  7. Said Ndemla
  8. Mwinyi Kazimoto
  9. Mussa Mgosi
  10. Hamisi Kiiza
  11. Peter Mwalyanzi
Wachezaji wa akiba ni
1. Angban Vicent
2. Said Issa
3. Simon Serenkuma
4. Emery Nimubona
5. Boniface Maganga
6. Pape Ndaw
7. Issa Ngoah

Pichaz za mwanzo kutoka uwanja wa Mkwakwani Tanga African Sports Vs Simba

September 12 ni siku ambayo Ligi Kuu Tanzania bara itazinduliwa rasmi kwa michezo kadhaa kupigwa, lakini millardayo.com inakuweka karibu na moja kati ya michezo ya Ligi Kuu. African Sports ya Tanga inaikaribisha Simba Sports Club ya Dar Es Salaam hii ndio habari ya mjini kwa hapa Tanga.
Nakusogezea pichaz 22 za mwanzo kutoka Uwanja wa CCM Mkwakwani
DSC_0002
DSC_0003
DSC_0004
DSC_0005
DSC_0007
DSC_0008
DSC_0009
DSC_0011
DSC_0012
DSC_0017
DSC_0018
DSC_0019
DSC_0022
DSC_0024
DSC_0026
DSC_0027
DSC_0031
DSC_0033
DSC_0041
DSC_0042
DSC_0043

 

 


 


 



 

 

Share on Google Plus

About Unknown

TEAM TASABA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment