Aunt Ezekiel, Wolper, Shamsa Ford walivyojitokeza kwenye mkutano wa ukawa August 27
2015 ni mwaka wa headlines za Uchaguzi
ambapo leo Agosti 27 Baraza la Wanawake Chadema (BAWACHA) walifanya
mazungumzo na mgombea Urais kupitia UKAWA, Mhe. Edward Lowassa.
Mkutano huo ulifanyika katika ukumbi wa
Millennium tower na kuhudhuriwa na mastaa wa bongo movie akiwemo,
Jackline Wolper, Aunt Ezekiel, Shamsa Ford na wengineo.
Hizi ni sababu za Justice Majabvi wa Simba kukataa kuchezea taifa lake…
Kiungo wa kimataifa wa Zimbabwe ambaye ametua Simba msimu huu akitokea klabu ya Vicem Hai Phong F.C ya Vietnam Justice Majabvi ambayo alikuwa amemaliza mkataba wake katika klabu hiyo. Bado anaendelea kukupa ile exclusive interview aliyofanya na millardayo.com.
Majabvi amesajiliwa na Simba kwa kiwango kizuri alichokionyesha baada ya kufanya majaribio na klabu hiyo ila swali lilikuwa hivi mbona Majabvi ana kiwango kizuri ila rekodi zinaonesha mara ya mwisho kucheza katika timu ya taifa ya Zimbabwe ni mwaka 2012, tatizo nini?
“Ndio
niliacha kuchezea timu ya taifa kwa sababu ya matatizo mengi katika timu
ya taifa, nimecheza timu ya taifa toka mwaka 2004 hadi 2012, kwa sababu
ya matatizo binafsi na shirikisho la soka la Zimbabwe, nilikuwa natumia
hela yangu kama nauli kuja kucheza timu ya taifa lakini sikuwa
nikirudishiwa” >>> Majabvi
Everton wamejibu ombi la John Stones kuuzwa Chelsea.
Siku mbili baada ya mchezaji wa kimataifa wa England anayekipiga katika klabu ya Everton, John Stones, kuandika barua ya kuomba kuuzwa na klabu yake, hatimaye klabu yake imejibu maombi yake.
Kupitia taarifa rasmi iliyotolewa jioni ya Alhamisi na mwenyekiti wa klabu ya Everton Bill Kenwright, ombi la mchezaji huyo kuuzwa kwenda Chelsea limekataliwa.
Mabingwa wa Uingereza, Chelsea wameshatuma ofa tatu tofauti kwenda Everton ili kumsajili Stones – walianza na ofa ya £20million, kisha £26m na wiki iliyopita £30m na zote zikapigwa chini, na sasa wanategemewa kurudi na ofa ya nne ya £33m.
‘Tangu lilipofunguliwa dirisha la usajili, tumeshakataa ofa nyingi kutoka kwa vilabu tofauti vya Premier League.
‘John hauzwi na ataendelea kubaki hapa kama mmoja wa wachezaji wetu muhimu wa kikosi cha kwanza’
Sentensi za mgombea Urais 2015 kupitia CCM Dkt Johh Pombe Magufuli
Mgombea wa Urais kupitia chama cha Mapinduzi, Dkt John Pombe Magufuli bado anaendelea na ziara zake za Uchaguzi 2015, huko mikoani.Sasa hapa nina sentensi za mgombea huyo akiwa ana zungumza katika ziara hizo.
Mtu wangu wa nguvu ninayo ripoti kutoka Uturuki waliko weka kambi Taifa Stars
Timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars bado ipo nchini Uturuki inaendelea na kambi yake ya siku nane kujiandaa kabla kucheza mechi dhidi ya timu ya taifa ya Nigeria Super Eagles ya kuwania kufuzu AFCON 2017, mchezo utakaopigwa Septemba 5 katika Uwanja wa Taifa Dar Es Salaam.
August 27 kocha wa Taifa Stars Charles Boniface Mkwasa ametoa ripoti kuhusu maendeleo ya kambi hiyo sambamba na hali za wachezaji, Mkwasa amethibitisha wachezaji kuwa katika hali nzuri kasoro Abdi Banda ndio anasumbuliwa na misuli. Vipi kuhusu uamuzi wa kuweka kambi Uturuki ikiwa kuna hali ya hewa ya baridi ukilinganisha na sehemu utakapopigwa mchezo huo.
“Kwa
ujumla kambi inaenda vizuri wachezaji wapo vizuri kasoro Abdi Banda ndio
amepata matatizo ya misuli, tupo huku kwa kambi tunajua kuna baridi ila
sehemu yenye baridi kuna Oxygen ndogo hivyo mapafu yanafanya kazi sana
kutafuta hewa hivyo ukizoea kuvuta hewa kidogo ukija katika sehemu
ambayo ina hewa nyingi inakuwa rahisi kucheza vizuri”>>> Mkwasa
0 comments :
Post a Comment