TASABA TOP HEADLINES OF THE DAY

Maneno ya Waziri wa Fedha kuhusu fedha zilizotumika kuboresha Miundombinu

.
.
Agosti 25 ni siku ambayo Waziri wa Fedha Saada Mkuya Salum alizindua bodi ya PPF na mafao mapya ya mfuko huo.Katika mazungumzo ya Waziri huyo pia alitoa ufanunuzi kuhusiana na fedha za mfuko wa jamii zilizotumika katika kuboresha miundombinu.
‘Na mimi kama msimamizi wa wizara ya fedha nina wajibu wa kujitolea maelezo kuhusiana na madeni ya mifuko ya hifadhi ya jamii, sisi Serikali ama hazina pale tumeunda kikosi kazi kwanza tuseme hatukuweza kulipa haya madeni kwasababu tulikuwa tumekwenda katika utaratibu wa kiserikali ni lazima maamuzi ya jinsi gani madeni haya yatalipwa katika baraza la Mawaziri’ – Saada Mkuya
.
Mratibu wa Kanda za Mfuko wa Pensheni wa PPF, Mbaruku akielezea namna fao hilo lilivyozingatia Mwanachama na Mwenza wake.
‘Kwa hiyo tulikuwa katika process lazima waraka uandaliwe na unaandaliwa katika ngazi ya chini kabisa lakini baada ya kufanyiwa marekebisho kwasababu inakwenda inaangaliwa inapewa comment, inafanyiwa marekebisho baada ya hapo imekwenda katika kikao cha makatibu wakuu baada ya kutolewa ufafanuzi baadhi ya maswali ama kuboreshwa zaidi  waraka ule ukawasilishwa katika Baraza la Mawaziri’ – Saada Mkuya

3X6A5632
.
Na kweli  siku ambayo tulikuwa tumekaa katika baraza la Mawaziri  mada ilikuwa ni hiyo moja tu ni lazima tuangalie ishu ya ulipaji wa mfuko ya pension napenda kuwahakikishia kwamba tumetoka na jawabu na  muongozo mzuri  na tulikuwa na timu ambayo inaangalia jinsi gani tunaweza tukatoa bond‘ -Saada Mkuya
.
Waziri Saada Mkuya akimpongeza Mwanachama wa PPF, Sara Jonas Haule, baada ya kumkabidhi shilingi milioni moja ikiwa ni malipo ya fao la uzazi.
‘Na hizi fedha lazima wananchi wakumbuke tulizitumia kweli tulikopa lakini tumekopa kwa madhumuni mazima ya kuendeleza miundombinu mbalimbali ya nchi hii, tumejenga Barabara, tumejenga Madaraja, tumejenga na sehemu nyingi.kwahiyo tulizitumia  kwaajili ya kuweka miundombinu ya kiuchumi lakini vile vile kwasababu hizi  ni fedha za wanachama ni lazima tuangalie utaratibu wa jinsi gani kuzirudisha fedha hizo’ – Mh.Saada Mkuya

Wizara ya Afya imetoa Idadi kamili na maeneo wanayotoka waathirika wa ugonjwa wa kipindupindu

.
.
NI Ugonjwa ambayo umechukua headline sana kwa mwaka huu, sasa leo Mh. Dr.Seif Selemani Rashid kutoka wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii aliitisha mkutano wa waandishi wa habari kuzungumzia idadi na maeneo wanayotoka waathirika wa ugonjwa wa Kipindupindu.
Kwa mujibu wa Waziri huyo alisema..‘Ndugu ya Wananchi Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii inapenda kutoa taarifa kwa umma kuhusu hali ya ugonjwa Kipindupindu  ambao umejitokeza katika mkoa wa Dar es Salaam na Morogoro, ugonjwa wa kipindupindu kwa mkoa wa Dar es Salaam ulianza katika manispaa ya Kinondoni kuanzia tarehe 15 mwezi wa nane mwaka huu, na hadi sasa Manispaa tatu zimeathirika kwa ugonjwa huu’ – Dr Seif
.
.
Aidha kwa Mkoa wa Morogoro ugonjwa ulianza tarehe 17 mwezi wa nane mwaka huu 2015, Kipindupindu ni Ugonjwa hatari unaoambukizwa kwa kula chakula au kinywaji chenye vimelea vya Ugonjwa “Vibrio cholera”ambavyo usababisha ugonjwa wa Kipindupindu, vimelea hivyo upatikana kwenye kinyesi, matapishi ya mgonjwa mwenye ugonjwa wa Kipindupindu au kwenye kituo chochote kilichochafuliwa na mgonjwa’ – Dr Seif
Ugonjwa huu unaweza ukasambaa kwa haraka iwepo kanuni za Afya hazitazingatiwa kama ifuatavyo ni kanuni hizo ambazo ninazitaja sasa ni zile zinazopelekea kupata Ugonjwa huo
1.Kutokunawa mikono kwa maji yanayotiririka na sabuni kabla ya Kula au baada ya kutoka Chooni
2.Kula chakula kilichoandaliwa katika mazingira yasiyo safi na Salama
3.Kunywa maji yasiyo safi na salama
4.Kumuhumia  mgonjwa mwenye dalili za ugonjwa huu bila kuzingatia kanuni za Afya juu ya kuepuka kupata maambukizi.
5.Waandaji  na upikaji wa Chakula bila kuzingatia kanuni za Afya’ – Dr Seif
.
.
6.Usafirishaji Olela kwa wagonjwa  wanaohisiwa kuwa wana Ugonjwa wa Kipindupindu ni vema kutoa taarifa iwepo kuna abiria mwenye dalili za ugonjwa huu ushauri namna ya kumsafirisha kwa namba ya Simu -0767300234 ili ushauri uweze kutolewa
Tangu ugonjwa wa Kipindupindu uanze tarehe 15 mwezi wa nane mwaka huu hadi kufikia tarehe 24 jana idadi ya wagonjwa walioripotiwa kwa mkoa wa Dar es Salaam ni 230 na vifo vya watu 7.
Idadi ya wagonjwa katika manispaa ni kama ifuatavyo
1.Kinondoni ni wagonjwa 186
2.Ilala ni wagonjwa- 22
3.Temeke ni wagonjwa 22
.
.
Aidha wagonjwa waliopo kwenye kambi za matibabu kwa tarehe ya jana 24 mwezi wa nane mwaka huu ni wagonjwa 71 mburahati 47, Buguruni wagonjwa 15 na Temeke wagonjwa 9′ – Dr Seif
‘Kwa taarifa zilizotufikia leo kwamba wagonjwa ambao wapo kwenye vituo vyetu hii leo katika jiji la Dar es Salaam ni wagonjwa 92, Kinondoni kukiwa na wagonjwa 65, Ilala wagonjwa 16 na Temeke wagojwa 11’ – Dr Seif
.
.
‘Katika Manispaa ya Kinondoni wagonjwa wengi wanatoka, Makumbusho, Kimara, Tandale,Goba, Kibamba, Manzese, Magomeni, Mwanyamala, Kijitonyama,Kigogo na Mburahati’ – Dr Seif
‘Katika manispaa ya Ilala maeneo yaliyoathirika au wanapotokea wagonjwa wenye vimelea vya Ugonjwa wa Kipindupindu yakiwemo Buguruni, Tabata, Chanika, Shaurishamba na Ilala, Katika manispaa ya Temeke ni Mtoni kwa Azizi Ally, Keko, na Yombo Vituka’- Dr Seif

Polisi wazuia ziara za Lowassa zisizo rasmi Dar es Salaam….

.
.
Jeshi la polisi kanda maalum ya Dar es salaam limepiga marufuku wagombea wa vyama vya siasa kufanya vitendo vinavyo hatarisha usalama wa raia na mali zao kwa kufanya mikusanyiko isiyo rasmi kwenye masoko na vituo vya daladala.
Kwa mujibu wa kamanda wa Polisi kanda maalum ya Dar es Salaam Suleiman Kova.. ‘Sasa kuna jambo limejitokeza ambalo limetulazimisha sisi jeshi la Polisi kupiga marufuku wagombea mbalimbali wa vyama katika uchaguzi huu hususani wale wenye nafasi ya Urais kwa vitendo vyao au kwa mtindo ambao umeibuka sasa hivi wa kwanza kutembelea maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam kama vile vituo vya Daladala, Masoko, ndani ya Daladala au Mabasi yoyote yale – Kova
.
.
‘Na hii inasemakana kwasababu ya kujua matatizo ya watu ambao wenye kipato cha chini inawezekana nia ni nzuri sana lakini sisi hapa atuzungumzia siasa au Uchumi  hapa tunazungumzia suala la Usalama kutokana na uzoefu uliojitokeza kwa zoezi hilo ni kwamba hilo zoezi sio la rasmi pia ziara hizo zinasababisha mikusanyiko mikubwa  isiyo ya lazima katika hali ambayo inaashiria kutokuwepo kwa Amani – Kova
3X6A5695
.
‘Wakati wa ziara wa aina hizo wamejitokeza makundi tofauti ya watu wakiwemo, waendesha Bodaboda wengi,  watu wa Daladala wengi wanajitokeza sawa wanashangilia  lakini kwa watu wengine ambao wasio wa makundi hayo ni kwamba inakuwa inaleta taharuki, hofu,  usumbufu, kuna kuwa na makelele mengi,  msongamano wa magari,  au hata kusimamisha usafiri katika  eneo hilo ambalo mgombea anakuwepo nasema kwamba inawezekana huyo mgombea kuna faida anayoipata lakini yeye kupata faida peke yake haitoshi kama suala la usalama alizingatiwa’ – Kova
.
.
‘Kwa mfano leo tarehe 25 mwezi wa nane ilibidi RPC wa kamanda Polisi Mkoa wa Ilala, Lucas Mkondya alilazimika kukutana ana kwa ana na Mgombea Urais kupitia Chadema, Edward Lowassa saa sita mchana watu walikuwa wamejaa pale katika mtaa wa Congo nadhani na Uhuru misongamano ya Magari mengi, Pikipiki wananchi wakalalamika kwamba ni nini sasa kinatokea na unajua Dar es Salaam ukisimamisha magari  kutokana na kundi lako kubwa basi litawaathiri Wananchi’ – Kova

Hizi ni picha za Mesut Ozil na Miss Uturuki zinazozua hofu kuhusu ukaribu wao

AMINE-GULSE
Miss Uturuki Amine Gulse
Picha ambazo zimekuwa zikizunguuka katika vyombo vya habari mbalimbali Uturuki zikimuonesha kiungo wa kimataifa wa Ujerumani anayeichezea klabu ya Arsenal ya Uingereza Mesut Ozil ameonekana akiwa na miss Uturuki kitu ambacho kinazua maswali mengi huenda wanamahusiano ya Kimapenzi.
mesut-ozil-getty_2830088b
Taarifa hizo zinakuja ikiwa masaa kadhaa yamepita  toka beki wa zamani wa klabu ya Manchester United Gary Neville ahoji kuhusu mchango wa kiungo huyo katika klabu ya Arsenal ya Uingereza kabla ya mechi ya Liverpool dhidi ya Arsenal ambayo ilimalizika kwa 0-0.
PAY-Mesut-Ozil (1)
PAY-Mesut-Ozil

Behind the scenes ya video mpya ya Future ‘Where Ya At’ feat Drake isikupite mtu wangu. 

fut22
Siku chache zilizopita niliisogeza kwako video mpya ya FutureWhere Ya At‘ aliomshirikisha rapper ,wemgome maarufu Drake. Lakini baada ya video hiyo kutoka na kupokelewa vizuri na mashabaiki, Future kanona bora aendelee kutupa burudani
Rapper huyo karudi tena wiki hii kuweka headlines zake kwenye kurasa za burudani, anaisogeza  kwetu behind the scenes ya video yake mpya.

Rasmi Juventus wamsajili nyota huyu kutokea Chelsea

Klabu ya Juventus ya Italia bado inaongeza nguvu katika kikosi chake kwa kusajili wachezaji kadhaa ili kuweza kuendana na kasi ya michuano mbalimbali itakayoshiriki msimu huu. Juventus ambayo imeondokewa na nyota kadhaa kikosini mwake ikiwemo Carlos Tevez na Andre Pirlo imeongeza nguvu katika kikosi chake.
IMG_20150825_182808
Juventus August 25 wamekamilisha usajili wa mkopo wa muda wa mrefu kwa aliyekuwa winga wa klabu ya Chelsea Juan Cuadrado ambaye alijiunga na Chelsea mwaka 2015 akitokea katika klabu ya Fiorentina ya Italia.
Pichaz Juan Cuadrado alivyowasili Italia August 24 kabla ya August 25 kutangazwa kusajiliwa
2BA2EA6200000578-0-image-a-85_1440458586550
2BA2EA5500000578-0-image-a-83_1440458491736

 


 

 


 


 


 

Share on Google Plus

About Unknown

TEAM TASABA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment