TASABA HABARI ZA SIASA

Freeman Mbowe kuhusu Dk. Slaa… Mrithi wa Jimbo la Lowassa? Waliogoma kusaini matokeo? Udiwani wa Manji na Said Fella..

dont-missout
MWANANCHI
Binti wa Waziri mkuu wa zamani, Edward Sokoine ambaye anaitwa Namelock Sokoine ameshinda kura za maoni kugombea ubunge Jimbo la Monduli kupitia CCM huku mkwe wa Lowassa, Siyoi Sumari akishindwa Jimbo la Arumeru Mashariki.
Namelock ambaye ni mbunge wa Viti Maalumu CCM alipata kura 29,582 akifuatiliwa na Loota Sanare aliyepata kura 8,809 na nafasi ya tatu, ilichukuliwa na Lolinyu Mkoosu aliyepata kura 235 na Payani Leyani akipata kura 226.
MWANANCHI
Wadau wawili wa michezo na burudani Tanzania Yusuf Manji na Said Fella wameibuka kidedea katika kinyang’anyiro cha udiwani katika jimbo jipya la Mbagala jijini hapa.
Manji ambaye ni Mwenyekiti wa Klabu ya Yanga na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Quality Group, alishinda katika Udiwani katika Kata ya Mbagala Kuu wakati Fella ambaye ni msimamizi wa kazi za wasanii na muasisi wa Kundi la Mkubwa na Wanawe, akishinda katika Kata ya Kilungure.
Fella ni Meneja wa mwanamuziki maarufu nchini, Diamond Platnumz, TMK Family na Yamoto Band.
Kaimu Katibu CCM Wilaya ya Temeke, Rutami Masunu alisema uchaguzi huo ulikwenda vizuri katika maeneo mengi isipokuwa kulitokea changamoto kidogo katika kata moja ambayo itafanya uchaguzi leo.
MWANANCHI
Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe amezungumzia kukosekana kwa Katibu Mkuu wa Chama hicho, Dk Willibrod Slaa katika vikao vya chama hicho vinavyoendelea, >>> “Nitazungumzia suala hilo muda muafaka ukifika… Siwezi kusema zaidi ya hapo”- hilo ndio jibu lake alipoulizwa.
Kauli hiyo ya Mbowe haikuondoa wingu zito lililotanda CHADEMA baada ya kutoonekana hadharani kwa kiongozi huyo katika matukio manne muhimu ya chama hicho kikuu cha upinzani, tangu Waziri Mkuu Wa Zamani, Edward Lowassa ajiunge nacho.
Naibu Katibu Mkuu (Bara), John Mnyika alionekana jana kwa mara ya kwanza katika kikao hicho na kufuta uvumi uliokuwa umesambaa kuwa alikuwa na mpango wa kuachana na CHADEMA kama inavyodaiwa kwa Dk Slaa.
Viongozi hao walianza kutoonekana katika shughuli za chama tangu Lowassa alipojiunga na Chadema Julai 28 na kukabidhiwa fomu ya kugombea Urais Julai.
Suala la kutokuwapo Dk Slaa ni kitu cha kawaida, anafanya kazi nyingine huko, lakini pia kuna wasaidizi wake hapa ambao ni sisi manaibu. Mlikuwa mnazungumzia Mnyika naye haonekani, si huyo. Hatuwezi kuendelea kujibu ‘rumors’ (uzushi) wa kwenye mitandao… nyie subirini si tupo mtaona kama yupo au la”– Naibu Katibu Mkuu Zanzibar, Salum Mwalimu.
Mbunge Mnyika alionekana katika viwanja vya hoteli hiyo lakini alikataa kuongelea chochote >>>“Siwezi kuzungumza chochote”—Mnyika.
NIPASHE
Wagombea wawili wa kiti cha Ubunge katika Jimbo la Moshi Mjini kwa tiketi ya CCM, ‘wamegoma’ kusaini matokeo ya kura za maoni yaliyompa ushindi mfanyabiashara maarufu wa Dar es Salaam, Davis Mosha.
Waliogoma kusaini matokeo hayo ni Buni Ramole na Patrick Boisafi, ambao walikuwa washindani wakuu wa Mosha kati ya wagombea 12 waliojitokeza kuomba kuteuliwa na CCM kugombea Ubunge Jimbo la Moshi Mjini.
Katibu wa CCM Moshi Mjini, Loth Ole Nessele amesema Buni alikataa kusaini matokeo hayo akidai amepata `presha’ kutokana na mchakato huo wakati Boisafi alimweleza kwamba hawezi kusaini kwa sababu yupo nyumbani peke yake na amechoka kutokana na mchakato huo.
Ni kweli nimekataa kusaini matokeo na tayari nimewaandikia na kuwakabidhi CCM barua nikiwaeleza kuhusu uamuzi wangu. Rushwa za wazi wazi na upendeleo kwa mgombea mmoja ni hatari na wala CCM isifikiri kwa mwendo huu italikomboa Jimbo la Moshi Mjini”– Buni Ramole.
NIPASHE
Baadhi ya Vigogo wakiwamo Mawaziri, Wabunge  wameangushwa katika Kura za Maoni za kutafuta wagombea Ubunge kupitia CCM.
Miongoni mwa waliangushwa ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe.
Wamo pia Manaibu Mawaziri wa Mambo Ya Ndani ya Nchi Na Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, mawaziri wa zamani, Mkuu wa Mkoa na wabunge.
Kwa upande wa Zanzibar, Wabunge na wawakilishi wa CCM wanaotetea tena nafasi hizo wengi wamejikuta wakianguka.
Wabunge na wawakilishi hao waliotupwa katika kura hizo yumo Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mahadhi Juma Maalim, aliekuwa akigombea Ubunge jimbo la Paje wilaya ya Kusini Unguja.

Huyu ndio msichana ambae anasoma PhD India na umri wake ni miaka 15 tu…!!

India
Sushma Verma na wazazi wake siku ya Graduation yake akimaliza Masters.
Kwa hesabu ya kawaida tu, mtoto anaanza Shule ya akiwa na miaka sita, au saba hivi… alafu mpaka kumaliza anakuwa na kama miaka 14, sasa kuna mtu kwenye umri huo alikuwa kamaliza high school na alikuwa Chuo tayari anamaliza zake degree!!
india-child-prodigy
Anaitwa  Sushma Verma ni msichana ambaye umri wake ni miaka 15, aligraduate Degree ya Microbiology Chuo cha Lucknow kilichopo India na kajiunga Babasaheb Bhimrao Ambedkar University (BBAU) kwa ajili ya kusomea Masters, kamaliza mwezi June 2015 na anaendelea kujipanga ili kuendelea na masomo ya PhD.
India II
Hii ilikuwa wakati Sushma Verma anasoma Masters, alikuwa na miaka 13 tu.. kuna wakati baba yake ilibidi atumie baiskeli kumsindikiza mwanae shule.

Sushma amewashangaza wengi lakini ndio hivyo, ana uwezo mkubwa sana darasani kitu ambacho Mkuu wa Chuo hicho amemuahidi kumpa ofa ya kulipiwa ada pamoja na Hostel bure akianza PhD ya environmental microbiology >>> “Lazima tumpe moyo kwa kipaji chake, tutamsajili na kumpatia Hostel na scholarship pia” >>> Prof. R C Sobti, Makamu Mkuu wa Chuo Babasaheb Bhimrao Ambedkar University.

Maneno ya Steve Nyerere baada ya kushindwa kwenye kura za maoni

Stori ninayokusogezea ni hii kutoka kwa msanii wa filamu Tanzania, Steve Nyerere ambaye wiki iliyopita hakufanikiwa kuwania ubunge wa jimbo la Kinondoni kutokana na kura zake kuwa chache.
Sasa leo msanii huyo amefunguka baada ya kukutana na ripota wa millardayo.com & AYO TV na kusema ‘Kwanza namshukuru Mwenyezi Mungu lakini niwashukuru Wananchi wa wiliaya ya  Kinondoni wamenionesha upendo ambao sikutarajia kwao, la pili sikubahatika kulishika gurumo hili la kuwa kiongozi na sitaweza kukata tamaa kwasababu hivi vitu vinahitajika uvumilivu kidogo,  siasa inahitaji kuwa mvumilivu na kila kitu kinachofanywa kama mwanadamu kinachotaka kupigiwa kura au kutafuta maisha ni uvumilivu unaohitajika kusonga mbele’ – Steve Nyerere
.
.
‘Kwasasa nipo kidogo mapumziko nikitafakari kuna yale niliyoyafanya na changamoto nilizozipata katika uchanguzi huo nimejifunza mambo mengi mengi ambayo kwangu yanatija kwa hiiyo kwangu ni changamoto kubwa sana’ – Steve Nyerere
.
.
RipotaTZA:Kuna taarifa tumezisikia kuwa kuna baadhi ya wasanii wameama kutoka chama cha mapinduzi na kwenda Chadema hizi taarifa zikoje?
Steve Nyerere...’Kwanza wao sio wavumilivu pili wamezaliwa na kukikuta chama cha Mapinduzi  vile vile kama wasanii hapa tulipofika ni msaada mkubwa sana wa mh.Rais Jakaya Mrisho Kikwete kutuonesha thamani yake kubwa kwetu ameweza kutukanwa kwaajili yetu na ameweza kututhamini, sasa leo na mimi nasikia kuwa kuna watu 15 wakiwemo wasanii wa bongo movie na wasanii wa Bongo Fleva 3 wamekiama chama cha CCM na kuhamia  CHADEMA’
.
.
‘Mimi nasema milango iko wazi watajichuja watabaki sahihi ambao ni sisi, na mtu kama mimi sina mawazo kwasababu nimeshindwa kura za maoni niseme kwamba nihamie chama Fulani sina mawazo hayo na sitarajii kuhama mimi nimezaliwa ndani ya chama cha Mapinduzi na nitakufa ndani ya chama cha Mapinduzi na ni chama changu nakipenda kwa dhati na pia nawambia wenzangu wakishindwa huko watarudi tu kwenye chama hiki cha Mapinduzi’ -Steve Nyerere

Dakika tisa za Freeman Mbowe kuhusu Dk. Slaa kutoonekana Vikao vya CHADEMA…

Mbowe II
Toka July 28 2015 siku ambayo Waziri Mkuu wa zamani na Mbunge wa Monduli Edward Ngoyai Lowassa alitambulishwa kujiunga CHADEMA na kukabidhiwa Kadi ya Chama hicho, zikaanza kuandikwa headlines Magazetini baada ya kutoonekana kwa Dk. Slaa katika Vikao mbalimbali vya Chama hicho.
SLAA

 


 


 


 

Share on Google Plus

About Unknown

TEAM TASABA
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment